dcsimg

Mnyama ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Wanyama (jina la kisayansi ni animalia na hutoka katika Kilatini) ni viumbehai wasio mmea, kuvu, bakteria, protista au arkea. Vile vile tunaweza kusema wanyama ni viumbehai wanaotegemea chakula kutoka sehemu nyingine: wao hawana uwezo wa kujitengenezea chakula chao wenyewe kupitia usanisinuru (nishati ya jua) lakini kutoka kwa viumbehai vingine ama wanyama wengine au mimea.

Kufuatana na aina ya chakula tunatofautisha hasa wanaokula mimea wanaoitwa walamani au walamea (kwa Kiingereza: herbivorous) na wanaokula nyama wanaoitwa walanyama au wagwizi (ing. carnivorous). Kuna pia walavyote (ing. omnivorous) wanaoweza kula kila kitu, ama mimea ama wanyama wengine (ing. omnivorous).

Wanyama wanahitaji oksijeni kwa kupumua.

Wanyama walio wengi hutembea yaani hubadilisha mahali wanapokaa, kwa hiyo wanahitaji milango ya maarifa.

Sayansi inayochunguza wanyama huitwa zuolojia, ambayo ni tawi la biolojia.

Aina za wanyama ni nyingi sana. Mara nyingi aina zao zinatofautishwa kama ni wanyama wenye seli nyingi (metazoa) au seli moja (protozoa) tu.

Kuna wanyama wanaoishi peke yao, katika vikundi na jamii. Mfano wa wanyama wanaoishi peke yao ni kifaru au nyoka. Wanajumuika kwa tendo la kuzaa pekee. Mfano wa wanyama wa jumuiya ni simba wanaokaa na kuwinda pamoja. Ushirikiano unasaidia kupata chakula bora. Mfano wa wanyama katika jamii ni nyuki na wadudu wengine.

Upande wa mwili hata binadamu ni mnyama na kimaumbile anahesabiwa kati ya mamalia.

Binadamu hutofautisha mara nyingi

ingawa lugha hii hutumiwa tu kwa wanyama wakubwa zaidi, kwa kawaida wenye uti wa mgongo (kwa Kilatini: Chordata).

Viungo vya nje

Morpho didius Male Dos MHNT.jpg Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mnyama kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Mnyama: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Wanyama (jina la kisayansi ni animalia na hutoka katika Kilatini) ni viumbehai wasio mmea, kuvu, bakteria, protista au arkea. Vile vile tunaweza kusema wanyama ni viumbehai wanaotegemea chakula kutoka sehemu nyingine: wao hawana uwezo wa kujitengenezea chakula chao wenyewe kupitia usanisinuru (nishati ya jua) lakini kutoka kwa viumbehai vingine ama wanyama wengine au mimea.

Kufuatana na aina ya chakula tunatofautisha hasa wanaokula mimea wanaoitwa walamani au walamea (kwa Kiingereza: herbivorous) na wanaokula nyama wanaoitwa walanyama au wagwizi (ing. carnivorous). Kuna pia walavyote (ing. omnivorous) wanaoweza kula kila kitu, ama mimea ama wanyama wengine (ing. omnivorous).

Wanyama wanahitaji oksijeni kwa kupumua.

Wanyama walio wengi hutembea yaani hubadilisha mahali wanapokaa, kwa hiyo wanahitaji milango ya maarifa.

Sayansi inayochunguza wanyama huitwa zuolojia, ambayo ni tawi la biolojia.

Aina za wanyama ni nyingi sana. Mara nyingi aina zao zinatofautishwa kama ni wanyama wenye seli nyingi (metazoa) au seli moja (protozoa) tu.

Kuna wanyama wanaoishi peke yao, katika vikundi na jamii. Mfano wa wanyama wanaoishi peke yao ni kifaru au nyoka. Wanajumuika kwa tendo la kuzaa pekee. Mfano wa wanyama wa jumuiya ni simba wanaokaa na kuwinda pamoja. Ushirikiano unasaidia kupata chakula bora. Mfano wa wanyama katika jamii ni nyuki na wadudu wengine.

Upande wa mwili hata binadamu ni mnyama na kimaumbile anahesabiwa kati ya mamalia.

Binadamu hutofautisha mara nyingi

Wanyama wa pori au wanyamapori Wanyama wa kufugwa au Mifugo Wanyama wa nyumbani (Wanyama-kipenzi)

ingawa lugha hii hutumiwa tu kwa wanyama wakubwa zaidi, kwa kawaida wenye uti wa mgongo (kwa Kilatini: Chordata).

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri