dcsimg

Ufunda ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Funda, dagaa-donzi au dagaa ya gege ni samaki wadogo kiasi wa baharini wa familia Apogonidae katika oda Perciformes lakini spishi kadhaa zinaishi katika maji baridi, zile za jenasi Glossamia hasa.

Maelezo

Kwa kawaida funda ni samaki wadogo. Spishi nyingi huwa chini ya sm 10 na mara nyingi huwa rangi kali. Wanajulikana kwa mdomo wao mkubwa na kwa mgawanyiko wa pezimgongo katika mapezi mawili tofauti. Spishi nyingi huishi katika maji ya tropiki au nusutropiki, ambapo hukaa katika miamba ya matumbawe na nyangwa. Hawa ni samaki wa usiku na wanashinda mchana katika mianya ya giza ndani ya mwamba. Angalau baadhi ya spishi huatamia mayai yao ndani ya mdomo wa madume.

Spishi za Afrika ya Mashariki

Picha

Marejeo

  • Rashid Anam & Edoardo Mostarda (2012) Field identification guide for the living marine resources of Kenya. FAO, Rome.
  • Gabriella Bianchi (1985) Field guide to the commercial marine brackish-water species of Tanzania. FAO, Rome.

Viungo vya nje

Crystal Clear app babelfish vector.svg Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ufunda kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Ufunda: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Funda, dagaa-donzi au dagaa ya gege ni samaki wadogo kiasi wa baharini wa familia Apogonidae katika oda Perciformes lakini spishi kadhaa zinaishi katika maji baridi, zile za jenasi Glossamia hasa.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri