Mbweta ni ndege wakubwa kiasi wa jenasi Chlorophoneus, Malaconotus na Telophorus katika familia Malaconotidae. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara tu. Ndege hawa wana rangi kali kwenye kidari na tumbo, k.m. nyekundu, machungwa, njano au kijani. Mgongo wao ni rangi ya majani au zeituni kwa kawaida. Wana domo nene lenye ncha kwa kulabu. Hula wadudu hasa na vertebrata wadogo pia, mijusi kwa kawaida. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe mtini na jike huyataga mayai 2-4.
Mbweta ni ndege wakubwa kiasi wa jenasi Chlorophoneus, Malaconotus na Telophorus katika familia Malaconotidae. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara tu. Ndege hawa wana rangi kali kwenye kidari na tumbo, k.m. nyekundu, machungwa, njano au kijani. Mgongo wao ni rangi ya majani au zeituni kwa kawaida. Wana domo nene lenye ncha kwa kulabu. Hula wadudu hasa na vertebrata wadogo pia, mijusi kwa kawaida. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe mtini na jike huyataga mayai 2-4.