dcsimg

Fukusi ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Fukusi, vidungadunga au vipukusa ni wadudu wa familia ya juu Curculionoidea katika oda Coleoptera. Kuna familia 7 na moja, Curculionidae, ni baina ya familia kubwa kabisa yenye jenasi 6800 na spishi 83,000. Familia ya juu ina spishi 97,000. Pengine familia mbili nyingine zinatambuliwa, Platypodidae na Scolytidae, lakini siku hizi hupatiwa cheo cha nusufamilia, ijapokuwa njia ya maisha yao ya kupukusa katika ubao imegeuza umbo lao sana.

Maelezo

Sifa bainifu ya fukusi ni domo refu lenye sehemu za kinywa kwenye ncha yake. Ukubwa wao unatofautiana kutoka mm 1 hadi 40. Vipapasio vya spishi nyingi sana vimepindika kama kisugudi, lakini fukusi wa kimsingi wana vipapasio nyofu.

Lava za fukusi hula tishu za mimea, miti au viyoga au mbegu zao. Wapevu hula maua, matunda, mbelewele, viyoga na kwa nadra wadudu, kama vile wadudu-gamba.

Kama chakula

Lava za fukusi, zile kubwa hasa, huliwa mahali pengi pa dunia. Zinaweza kuliwa mbichi, zilizopikwa, zilizokaangwa au zilizobanikwa.

Spishi zilizochaguliwa za Afrika ya Mashariki

Picha

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Fukusi: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Fukusi, vidungadunga au vipukusa ni wadudu wa familia ya juu Curculionoidea katika oda Coleoptera. Kuna familia 7 na moja, Curculionidae, ni baina ya familia kubwa kabisa yenye jenasi 6800 na spishi 83,000. Familia ya juu ina spishi 97,000. Pengine familia mbili nyingine zinatambuliwa, Platypodidae na Scolytidae, lakini siku hizi hupatiwa cheo cha nusufamilia, ijapokuwa njia ya maisha yao ya kupukusa katika ubao imegeuza umbo lao sana.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri