dcsimg

Shore (Muscicapidae) ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Shore, shorwe au sholwe ni ndege wadogo wa nusufamilia Muscicapinae katika familia Muscicapidae. Spishi nyingine zinaitwa chekiro, kidaku au gongo shaba. Spishi kadhaa za familia Pycnonotidae zinaitwa shore pia. Wale wa Muscicapinae wana rangi ya kahawa, kijivu au nyeusi kwa kawaida, lakini spishi nyingine wana rangi kali kama buluu, nyekundu, manjano na machungwa. Shore wanatokea misitu na maeneo mengine yenye miti katika Afrika na Asia. Hula wadudu. Kwa kawaida shore hukaa tawi wakiangalia ujirani. Wakiona mdudu huruka ili kumkamata na kurudi tawi. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika tundu la mti au dhidhi ya shina. Jike huyataga mayai 2-6.

Spishi za Afrika

Spishi wa Asia

Picha

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Shore (Muscicapidae): Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Shore, shorwe au sholwe ni ndege wadogo wa nusufamilia Muscicapinae katika familia Muscicapidae. Spishi nyingine zinaitwa chekiro, kidaku au gongo shaba. Spishi kadhaa za familia Pycnonotidae zinaitwa shore pia. Wale wa Muscicapinae wana rangi ya kahawa, kijivu au nyeusi kwa kawaida, lakini spishi nyingine wana rangi kali kama buluu, nyekundu, manjano na machungwa. Shore wanatokea misitu na maeneo mengine yenye miti katika Afrika na Asia. Hula wadudu. Kwa kawaida shore hukaa tawi wakiangalia ujirani. Wakiona mdudu huruka ili kumkamata na kurudi tawi. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika tundu la mti au dhidhi ya shina. Jike huyataga mayai 2-6.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri